Taarifa ya Pato la Taifa Robo ya Pili ya Mwaka 2017
Thamani ya Pato la Taifa katika kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka 2017 kwa bei za soko za mwaka 2007 ilikuwa Shilingi trilioni 12.8 ikilinganishwa na Shilingi trilioni 11.9 ya thamani iliyopatikana katika kipindi kama hicho mwaka 2016, ambayo ni sawa na kasi ya ongezeko ya asilimia 7.8 ikilinganishwa na kasi iliyorekebishwa ya asilimia 8.5 ya mwaka 2016.