The United Republic of Tanzania

National Bureau of Statistics

Statistics for Development
DCP Kaziulaya Atembelea Maktaba ya NBS Dodoma
Posted On: 23 January, 2026
DCP Kaziulaya Atembelea Maktaba ya NBS Dodoma

Naibu Kamishna wa Magereza Makao Makuu Dodoma, DCP Justin Kaziulaya ametembelea Maktaba ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu iliyopo Makao Makuu ya Ofisi hiyo jijini Dodoma tarehe 22 Januari 2026. 

Pamoja na mambo mengine, DCP Kaziulaya ameridhishwa na namna Maktaba hiyo inavyofanya kazi ambapo Mkutubi, Issa Bernard Magabiro amemkabidhi machapisho ya Takwimu mbalimbali kwa ajili ya kupanga na kufanya maamuzi ya shughuli za kila siku za Jeshi hilo.