SG Dkt. Msengwa Afungua Kikao Uchambuzi IHBS 2025 Ikiwa ni Maandalizi ya Ripoti ya EAC - MPI
Mtakwimu Mkuu wa Serikali Ofisi ya Taifa ya Takwimu - NBS, Dkt. Amina Msengwa amefungua kikao kazi cha siku tano cha uchambuzi wa taarifa za Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania (Integrated Household Budget Survey - IHBS) za Mwaka 2025 kwa ajili ya kuandaa ripoti ya Umaskini Usiotokana na Kipato (Multidimensional Poverty Index - MPI) kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.