NBS, TASAC Zasaini Makubaliano Kufanya Sensa Vyombo vya Usafiri Majini
Ofisi ya Taifa ya Takwimu - NBS kwa kushirikiana na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania - TASAC, zimesaini Makubaliano ya Ushirikiano - MoU kufanya Sensa ya Vyombo vya Usafiri wa Majini na Wajenzi wa Meli Tanzania Bara Mwaka 2026/2027 ili kupata Takwimu rasmi zitakazosaidia kuboresha usimamizi na maendeleo ya sekta hiyo.