NBS, IHI Zaendesha Mafunzo Mifumo ya Taarifa za Kijiografia
Ofisi ya Taifa ya Takwimu - NBS kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti ya Ifakara - IHI zinaendesha mafunzo ya Mifumo ya Taarifa za Kijiografia katika Sekta ya Afya (Geospatial Modelling on Public Health) kupitia Mradi wa Malaria Atlas - MAP, kuwajengea uwezo watafiti na wataalamu kutumia mifumo hiyo katika kukusanya na kuchambua taarifa ili kuzalisha Takwimu rasmi.