NBS, OCGS Zaanza Majaribio Utafiti NPS 2026
Ofisi ya Taifa ya Takwimu - NBS kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar - OCGS zimeanza zoezi la majaribio kwa Wadadisi na Wasimamizi wa Utafiti wa Ufuatiliaji wa Kaya (National Panel Survey - NPS) 2026 katika Kijiji cha Nzihi, Kata ya Nzihi, Wilaya ya Iringa mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya kukamilisha mafunzo ya nadharia kabla ya kuanza utafiti rasmi nchini.