NBS, OCGS Zaanza Uandishi wa Ripoti Mbili Arusha
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), imeanza kikao kazi cha uandishi wa Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi nchini pamoja na Ripoti ya Umaskini Usiotokana na Kipato nchini za mwaka 2025, zoezi ambalo linafanyika kwenye Ukumbi wa Mafao Village, jijini Arusha.