NBS, OCGS Zaanza Uhakiki, Uchambuzi wa Taarifa Utafiti wa Sekta Isiyo Rasmi 2025
Ofisi ya Taifa ya Takwimu – NBS kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar - OCGS zimeanza uhakiki na uchambuzi wa taarifa za Utafiti wa Sekta Isiyo Rasmi wa mwaka 2025 kwa lengo la kupata takwimu bora zitakazoisaidia Serikali pamoja na wadau kupanga mipango ya maendeleo nchini hususan uratibu wa biashara zilizo kwenye sekta isiyo rasmi.