Wataalam NBS Waanza Zoezi la Uchakataji Maoni ya Wadau Maandalizi ya SP Mpya
Wataalam wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu - NBS wameanza zoezi la kuchakata maoni ya wadau wa Takwimu nchini kutoka sekta za umma na sekta binafsi baada ya kukamilika kwa zoezi la kupokea maoni ya wadau hao, kwa lengo la kuboresha rasimu ya Mpango Mkakati - SP wa Ofisi hiyo wa mwaka 2026/2027 hadi 2030/2031.