Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Taifa ya Takwimu

Takwimu kwa Maendeleo
Kuahirishwa Utangazaji wa Matokeo ya Utafiti wa Ajira na Mapato wa Mwaka 2022/23 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Imewekwa: 09 July, 2024

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS) zinapenda kuwataarifu watumiaji wa takwimu za ajira na mapato na umma kwa ujumla kuwa, matokeo ya Utafiti wa Ajira na Mapato (EES) wa Mwaka 2022/23 kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyo kusudiwa kutolewa tarehe 30 Juni 2024, sasa yatatolewa tarehe 30 Septemba 2024. Kuchelewa kwa matokeo hayo kumetokana na sababu za kiufundi. Ofisi za NBS na OCGS zinaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali wasiliana nasi kwa:

 

Mtakwimu Mkuu wa Serikali,

Ofisi ya Taifa ya Takwimu,

S.L.P 2683,

Dodoma.

Barua Pepe: sg@nbs.go.tz

Simu: +25526 - 296382